Monday, June 1, 2015

KATIBU MKUU MPYA WIZARA YA MAMBO YA NJE BALOZI LIBERATA MULAMULA AKABIDIWA OFISI RASMI



Katibu Mkuu Mpya wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akikabidhiwa rasmi Ofisi na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi John Haule. Kabla ya uteuzi huo Balozi Mulamula alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mhe. Haule kwa sasa ni Balozi wa Tanzania nchini Kenya. Makabidhiano hayo yalifanyika Wizarani leo tarehe 01 Juni, 2015.



Katibu Mkuu, Balozi Mulamula akiwa kwenye Mkutano na baadhi ya Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo mara baada ya kukabidhiwa rasmi Ofisi na Balozi Haule.


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Nigel Msangi (wa kwanza kulia), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga (wa pili kutoka kulia), Mkurugenzi Idara ya Sera na Mipango Bw. James Lugaganya na Balozi Haule wakimsikiliza Balozi Mulamula (hayupo pichani\

No comments:

Post a Comment