Monday, June 1, 2015

AJALI YA LORI LA MAFUTA YAUWA NAIGERIA



Nigeria imeendelea kukumbwa na matukio ya vifo, baada ya tukio la kundi la Boko Haram kuvamia msikiti na kuuwa watu 16 jana, kuna taarifa nyingine ambayo si nzuri kutoka nchini humo.
Watu wasiopungua 70 wamefariki dunia Mashariki mwa Nigeria baada ya lori la kubeba mafuta kushika moto huku magari mengine 15 nayo yakishika moto.
Mashuhuda wa ajali hiyo iliyotokea jana wamesema dereva wa gari hilo alishindwa kudhibiti mwendo kazi wa gari hilo ndipo likakosa mwelekeo na kutoka barabarani na kuwagonga watu waliokuwa wakisubiri usafiri katika kituo kimoja cha mabasi.

No comments:

Post a Comment