Sunday, April 20, 2014

REAL MADRID MANGWA LIGI KUU UHISPANIA COPA DEL REY



Bale asherekea bao la ushindi dhidi ya Barcelona

Timu ya Real Madrid ndio mabingwa wa mwaka huu wa kombe la Copa del Rey .

Madrid waliwacharaza wapinzani wao wa jadi katika ligi ya nyumbani La liga Barcelona mabao 2 kwa 1 katika fainali iliyochezwa jana mbele ya mfalme wa Uhispania .
Kocha wa Madrid Carlo Ancelotti alikuwa anajikuna kichwa kwani mshambulizi wake nyota Cristiano Ronaldo hakuwa uwanjani kutokana na jeraha la mguu na hivyo ikambidi kumchezesha mshambulizi aliyegharimu kitita kikubwa

zaidi msimu huu Gareth Bale .
Na alidhibitisha udedea wake alipofuma bao la ushindi zikiwa zimesalia dakika tano tu mechi hiyo kukamilika na hivyo kuisadia kutwaa taji lake la 19 la Kombe hilo la mfalme la Copa del rey.
Real Madrid ilidhibitisha niya yao mapema kwa bao la dakika ya 11 Angel Di Maria .


Real Madrid yasherekea ushindi dhidi ya Barcelona
Lakini ikasawazishwa na bao la Bartra katikadakika ya 68 ya kipindi cha pili.

No comments:

Post a Comment