Wednesday, September 9, 2015

DIAMOND ATAJWA ACHAGULIWA TENA KWENYE TUZO ZA KIMATAIFA



Msanii wa Bongo Flava Diamond Platnumz anazidi kuipeperusha bendera ya Tanzania, Tuzo nyingi sana zinazidi kutambua juhudi na kazi ya Diamond kwenye muziki wa Tanzania.


Good news kwako mtu wangu, mtu wetu Diamond Platnumz amepata nafasi nyingine kubwa ya kuiwakilisha Tanzania kwenye tuzo za kimataifa.



Tuzo za MTV Europe Awards maarufu kama MTV EMA kwa mwaka huu wa 2015 zimemtaja Diamond Platnumz kuwa miongoni mwa wasanii kutoka Africa wanaowania kipengele cha ‘Best African Act’, wasanii wengine waliobahatika kuingia kwenye kipengele hicho ni; Davido, AKA (South Africa) na Yemi Alade (Nigeria).



Yemi Alade ni msanii pekee wa kike kwenye kipengele hiki cha Best African Act.



Davido kutoka Nigeria


AKA kutoka South Africa.
MTV EMA 2015 inahitaji mtu wa tano kukamilisha orodha ya ‘Best African Act’ mtu wangu na kama wewe ni mdau mkubwa sana wa muziki mzuri basi MTV EMA 2015 inakupa wewe nguvu na kibali cha kumchagua mtu wa 5 unaehisi atafaa kuchuana na Diamond Platnumza na wengine kwenye kipengele hiki..




kwenye wale watano waliopendekezwa wapo; Wizkid, KO (South Africa), Stone Bwoy (Nigeria), Cassper na DJ Arafat.




Kumpata mmoja kati ya watano hapo juu, utaratibu wa kuwapigia kura upo hivi… unaandika #MTVEMA ikifuatiwa na hashtag (#Nominate) na jina la msanii na kisha unatweet mara nyingi uwezavyo kwenye Twitter ili kumpata yule unayeona anastahili kufunga kipengele hiki.




Tuzo za MTV EMA Awards 2015 zinafanyika tarehe 25 October jijini Milan, Italy. Mwisho wa kupiga kura ni tarehe 14 September 2015.

No comments:

Post a Comment