Monday, June 8, 2015

MILLARD, DIAMOND, SHERIA NGOWI, DK. MENGI, ZITTO WALAMBA TUZO KATIKA KONGAMANO LA WANAVYUO DAR




Dkt. Kitila Mkumbo akipokea tuzo ya mwanasiasa anayependwa sana na mwenye mvuto kwa jamii ambayo tuzo ilienda kwa Zitto Kabwe.



Mlezi Dkt. David Rweikiza akitoa tuzo kwa mwanamitindo anayependwa ambayo tuzo ilienda kwa Sheria Ngowi, alipokelewa na mwakilishi wake.



Mkurungezi wa Masoko wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa, akitoa tuzo kwa mtangazaji anayependwa ambayo tuzo ilienda kwa Millard, tuzo ilipokelewa na mwakilishi wake anayefahamika kwa jina la Askofu.
Mkurungezi wa AEG LTD, Iman Kajula akitoa tuzo kwa Diamond Platinumz kama msanii anayependwa, tuzo ilipokelewa na mwakilishi wake Nikki wa Pili.
Mkurungezi wa IPP Media, Dkt. Reginald Mengi akitoa shukrani kwa waandaaji wa tuzo hizo.
Washindi na wawakilishi wa tuzo mbalimbali zilizotolewa kwenye kongamano hilo.



Mwenyekiti wa Chama cha Wanafunzi wanaosoma Kitivo cha Masoko cha Chuo Kikuu UDSM (DUMA), Dkt. Ulimwengu akitoa historia fupi ya Tuzo za ACHIVERS AWARDS katika kongamano la wanafunzi wanaosoma Kitivo cha Masoko na Biashara lililofanyika Jumamosi iliyopita UDSM na kukutanisha wanataaluma wengi na wajasiriamali waliofanikiwa. Kongamano hili lilikutanisha vyuo mbalimbali ikiwemo UDSM, IFM, CBE, na TIA.


Mkurunezi wa IPP Media, Dk. Regnald Mengi akitoa hamasa ya wanafunzi kuweza kutumia fursa kuweza kutengeneza mawazo ya kibiashara katika kongamano la wanafunzi wanaosoma masomo ya Masoko na Biashara


Wanafunzi wakifuatilia kwa makini kongamano hilo la 'Marketing Forum'.


Washiriki wa kongamano wakionekana kushangilia baada ya Dk. Mengi kuwa anatarajia kuzindua kitabu chake kipya mwishoni mwa mwaka huu.
Mkurungezi na Mwanzilishi wa Mwanaharakati Mzalendo Media pia Mkurungezi Mtendaji wa Kajo Itech ambao walikuwa ni wadhamini rasmi wa kongamano hilo, Krantz Mwantepele akiongea na wanafunzi jinsi gani wanaweza kufungua fursa za baishara na kuweza kujiajiri kutumia mitandao ya kijamii.

(PICHA / HABARI: MWANAHARAKATI MZALENDO MEDIA)

No comments:

Post a Comment