Monday, July 21, 2014

MICROSOFT KUPUNGUZA AJIRA ELFU 18


microsoftkm 
Kampuni ya kiteknolojia ya Microsoft inatarajia kupunguza takribani ajira elfu 18 za wafanyakazi wake na kuweka rekodi ya kupunguza watu wengi zaidi katika historia ya kampuni hiyo kwa miaka 39.
Punguzo kubwa litafanyika kwa ajira elfu 12 kwa kitengo chake cha Nokia ambacho kampuni hiyo ilinunua mwezi Aprili.
Punguzo hilo ni kubwa tofauti na matarajio ya watu 6000 yaliyokuwepo awali.
Kampuni hiyo inaajiri watu laki moja na 27 dunia nzima ikiwa ni pamoja wa wafanyakazi 3,500 nchini Uingereza.
Kampuni hiyo imekataa kusema ni ajira kiasi gani zitapunguzwa nchini Uingereza ikiwa ni matokeo ya mabadiliko hayo.

No comments:

Post a Comment