Thursday, June 12, 2014

SOKO LA KARUME LA TEKETEA KWA MOTO USIKU WA LEO

 


Mabanda ya wamachinga eneo la Soko Karume yanaungua na moto.

Habari zaidi zitafuata.

Moto bado ni mkali, unazidi kusambaa na sasa unaelekea Breweries. Usipodhibitiwa mapema utaleta athari kubwa sana.

Hali bado ni tete, Fire walifika katika eneo la tukio na sasa wanaondoka bada ya kukubali kushindwa, hakuna wanachoweza kuokoa.

Nguzo za umeme zinaungua pia.

Kuna umati wa watu mkubwa, baadhi wanalia kwa uchungu wakiwa wamejishika kwa kukata tamaa.

Chanzo kinadaiwa kuwa ni sehemu ya "Mama Ntilie" (ambao inasemekana huchemsha maharage na kuyaacha usiku ili yaive vizuri)

 PICHA hizi zimepigwa na mwandishi wa JamiiForums:




No comments:

Post a Comment