Tuesday, June 10, 2014

MKENYA DIVORC ORIGI KUSHIRIKI KOMBE LA DUNIA CHINI BRAZIL

Divorc Origi ni mkenya na mwanaafrika mashariki wa kwanza kushiriki kombe la dunia
Mshambuliaji wa Lille ya Ufaransa , Mkenya Divorc Origi ambaye ni mzaliwa wa Ubelgiji ni miongoni mwa wachezaji wa timu ya taifa ambayo imeondoka Jumanne kuelekea Brazil kwa mashindano ya kombe la dunia kuanzia Alhamisi wiki hii.
Origi, mwanae Mike Okoth, mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Kenya Harambee Stars atakua mchezaji wa kwanza wa Afrika Mashariki kuiwakilisha Ubelgiji, na yuko pamoja na wachezaji nyota kama vile Vincent Kompany wa Manchester City na Eden Hazard wa Chelsea.
Watakabiliana na Algeria mechi yao ya kwanza ya kundi H Juni tarehe 17 na siku tano baadae wanapepetana na Urusi kisha Korea Kusini kwenye mechi za mchujo.
Akizungumza na BBC kwa njia ya simu akiwa Ubelgiji Origi anasema:'' Algeria ni timu yenye wachezaji wazuri kwa hivyo hatuwezi kuidharau. Tutacheza mchezo wetu wa kawaida lakini nina matumaini makubwa tutashinda.’’ Anasema Urusi na Korea pia si timu hafifu hasa Warusi. Lengo lake kubwa ni Ubelgiji kufuzu kwa raundi ya pili kisha kutoka hapo anasema mambo yatakuwa sawa kabisa.
Kuhusu mbona ameamua kuiwakilisha Ubelgiji na sio taifa la babake Kenya, Origi anasema alitilia maanani mambo mengi kama vile usimamizi mzuri wa kandanda nchini humo, mizizi yake ya kandanda iliyoko huko, marafiki, ushauri wa babake pamoja na Ubelgiji kufuzu kwa kombe la dunia kwani haijulikani ni mwaka upi Kenya itafuzu kwa kombe la dunia.

No comments:

Post a Comment