Tuesday, June 10, 2014

DIAMOND AFANYA KOLABO NA MAFIKI ZOLO SOUTH AFRIKA

2
Hapa ni kwenye gari safari ya kuelekea studio ndio inaanza, Mameneja Bab Tale kushoto na Salam kulia pembeni na Diamond
Hatimae mpango wa Mafikizolo wa South Africa ambao ni mastaa wa hit single ya ‘khona’ waliochukua tuzo mbili kwenye MTV Africa music awards 2014 kufanya kolabo na Diamond umefanikiwa kwenye usiku wa June 9 2014.
Diamond pamoja na mameneja wake wawili ambao ni Salam na Bab Tale waliongozana mpaka kwenye studio za msanii mkongwe aitwae Oskido ili kurekodi kolabo hiyo ya Mafikizolo, kundi la Afrika kusini lililorudi kwenye chati kupitia mikono ya Oskido.
3
Ndio tunawasili kwa Oskido, mtu wako wa nguvu nilikuepo kuhakikisha kila kinachotokea kinakufikia
Kama hukusikiliza Clouds FM Top 20 Jumapili ya June 8 2014, wakati wa kufanya mazoezi ya tukio la MTV kwenye tuzo za Mama Durban South Africa June 7 2014, Mafikizolo waliomba kurekodi wimbo na Diamond baada ya kushawishika kufanya nae kolabo hivyo wakaahidi kushughulikia gharama zote za kumuongezea Diamond muda wa kuendelea kukaa South Africa pamoja na kubadili ticket ya ndege ili wakamilishe kazi yao.

9
Oskido ni msanii mkubwa sana na mwenye uwezo hapa South Africa na anapendwa sana ila pamoja na ukubwa wa jina lake, huwa hajiweki juu kabisa… ni mpole na simple kila wakati, nakumbuka hapa yeye ndio aliomba kupiga picha na Diamond.
8
Diamond alipoingia studio alikua bado hajapewa topic ya wimbo, yani alikua hajui wimbo unahusu nini ila dakika kadhaa baadae akaanza kushusha mistari yake… alipoingia kuingiza voco ya kwanza Mafikizolo pamoja na Producer wakampigia makofi na kusmile kuashiria kijana katishaa.



Mafikizolo na Diamond
14
Upande mwingine ambao wengi hawaujui, Diamond ni mtani na anachekesha sana, ana aina yake ya kuhadithia kitu mpaka ukacheka… ilikua goodtimes studio kiukweli
CREDIT MILLARD AYO.

No comments:

Post a Comment