Saturday, May 24, 2014

LOUS SUAREZ KUTOCHEZA KOMBE LA DUNIA BRAZILI 2014


Hofu iwapo Suarez atacheza Brazil
Matumaini ya mashabiki wa Uruguay kuwa mshambulizi wa Liverpool ya Uingereza ataiongoza timu yao katika kombe la dunia yameingia ati ati baada ya mshambulizi huyo bora katika ligi kuu ya Uingereza kufanyiwa upasuaji wa dharura wa goti lake mapema leo.
Suarez aliyeisaidia Uruguay kumaliza katika nafasi ya nne katika kombe la dunia ya mwaka wa 2010 iliyokuwa huko Afrika Kusini alitarajiwa kushiriki katika safu ya mashambulizi lakini upasuaji huu unamaanisha hatoweza kushiriki katika maandalizi kwa jumla ya majuma matatu hivi.
Kulingana na ripoti za magazeti nchini Uruaguay mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 27 aligundua jumatano kuwa alikuwa na jeraha la goti na akalazimika kufanyiwa upasuaji wa kisasa kwa haraka kuambatana na ushauri wa muuguzi mkuu wa timu hiyo ya taifa.
Kulingana na daktari huyo mfumo uliotumika kwa operesheni hiyo ''arthroscopy'' itamruhusu Suarez kupata nafuu kwa takriban siku 15-20 na hivyo huenda akarejea kabla ya kuanza kwa kipute hicho cha fainali ya kombe la dunia .

Hofu iwapo Suarez atacheza Brazil
Shirikisho la soka nchini humo imetoa taarifa kwa vyombo vya habari huko Montevideo ikisema kuwa wanamtarajia nyota huyo wa Uruguay kurejea mapema .
Uruguay imeratibiwa kufungua kampeini yake dhidi ya Costa Rica mjini Fortaleza mnamo Juni 14

No comments:

Post a Comment