Sunday, April 20, 2014

NAHODHA WA MELI ILIYOZAMA KOREA KUSINI MBARONI


Nahodha wa kivuko cha Korea Kusini kilichozama na kusababisha watu zaidi ya 300 kutojulikana walipo amekamatwa Jumamosi (19.04.2014) kwa tuhuma za uzembe na kuwatelekeza watu waliokuwa kwenye shida ya kuhitaji msaada. Wapelelezi wamemkamata Lee Joon -Seok na wafanyakazi wenzake wawili mapema leo asubuhi na wote watatu wameshutumiwa kwa kuwatelekeza mamia ya abiria waliokuwa wamenasa ndani ya chombo hicho na kuhangaika wenyewe kujiokowa. Mahakama imesema imeamuru kukamatwa kwao ili kuzuwiya watuhumiwa hao kukimbia au kuharibu ushahidi.

Nahodha huyo mwenye umri wa miaka 68 yuko chini ya uchunguzi kwa kuwa miongoni mwa watu wa mwanzo kuitelekeza meli hiyo wakati abiria wake wakiwa bado wako hatarini.Lee amefunguliwa mashtaka ya uzembe na kushindwa kuhakikisha usalama wa abiria kinyume na sheria za bahari.Abiria waliambiwa kupitia vipaza sauti kwamba wabakie hapo walipo licha ya kuwa meli hiyo ilikuwa ikizama upande mmoja.

No comments:

Post a Comment