Saturday, April 5, 2014

MGOMBEA UBUNGE CHALINZE AJERUHIWA KWA MAPANGA.




MGOMBEA Ubunge katika Jimbo la Chalinze, wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, Ramadhani Mgaya (pichani juu) kupitia chama cha AFP amejeruhiwa kwa mapanga na watu wasio julikana.
Mgaya amesema amevamiwa na kujeruhiwa na mtu ambaye hamfahamu majira ya saa sita za usiku akiwa katika nyumba ya kufikia wageni ya Goodtime Chalinze.
"Nimevamiwa na kujeruhiwa na mtu ambaye simfahamu ahsante uongozi wa Chadema kwa kunisaidia," alisema Mgaya.
Mgaya amesema ameumia mikononi wakati akipangua nakujitetea maana mvamizi alikuwa na panga.
Mbali na yeye pia amesema kiongozi wa Chadema, Mwita Waitara naye alijeruhiwa kwa kuwa alikuwa mmoja ya watu waliokuwa wakimsaidia.
(Habari na Father Kidevu Blog)

No comments:

Post a Comment