Monday, March 31, 2014

JINSI ROMA MKATOLIKI ALIVYOUZA WIMBO WAKE KWENYE WHATSAPP

  
Inawezekana kama mitandao ya kijamii ukiitumia vizuri inaweza kukupatia faida kubwa kuna watu kadhaa ambao kupitia mitandao ya kijamii wanendesha maisha yao vizuri miongoni mwao kuna jamaa mmoja anajiita dalali Mkombozi aliwahi ku-amplify anavyoitumia Instagram kuendesha maisha yake.



Roma Mkatoliki leo ametoa idadi ya pesa alizowahi kuingiza kupitia wimbo wake wa 2030 ambao alianza kwa kuuza kupitia mtandao wa Whatsapp >>’2030 nilikua nauza kwa shilingi 3,000 kuna artist wanatoa album au mixtape ina nyimbo 20 anauza 5,000 ambao unakuta wanaongea huyo Roma ni nani anatoa wimbo anauza 3,000′

‘Badala ya kusaidiwa na wasanii wenzangu ndiyo wananikandia mi Tanga nina ofisi yangu na napokea album kibao nawauzia tu wana,unakuta watu wanaongea mbona wimbo wenyewe taarifa ya habari halafu anauza 3,000,kwa haraka haraka niliuza kama 1,400,000 kwa kipindi kile cha mwanzo’. Source 255 Clouds Fm

No comments:

Post a Comment