Thursday, November 27, 2014

WATANZANIA WAHIMIZWA KWENDA KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA KUPIGIA KURA



Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Jumanne Sagini akionyesha kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) Daftari la Wapiga Kura linalotumika kuandikisha wananchi katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Kushoto ni Mratibu wa Uchaguzi huo Bw. Denis Bandisa.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI Bw. Jumanne Sagini akitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga Kura ili waweze kushiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu. Pia Katibu Mkuu huyo amewataka Viongozi wote wanaosimamia uchaguzi huo kuzingatia sheria na kanuni za uchaguzi. Kushoto ni Mratibu wa Uchaguzi huo Bw. Denis Bandisa na kulia ni Afisa Mwandamizi wa TAMISEMI Bw. Mohamed Mavura.



No comments:

Post a Comment