Monday, June 9, 2014

RAIS WA WANAFUNZI SAUTI MWANZA AJIUNGA NA CCM

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wanachama wa Tawi la CCM SAUT Kambarage na wananchi wa Nyamalango ,wilaya ya Nyamagana Mwanza ambapo aliwaambia kuwa CCM itaendelea kuongoza kwani ndio chama pekee chenye sera inayoeleweka kwa wananchi,mipango na ahadi zake zinatekelezwa kila kona ya nchi.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akipokea kadi ya CHADEMA kutoka kwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo cha Mtakatifu Agustine Ndugu Simon Philbert Macheyeki ambaye amejiunga rasmi na CCM,katika mkutano huo zaidi ya wanafunzi 86 wa chuo hiko wamejiunga na CCM na wanachama wapya 420 wamejiunga na CCM.
  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimkabidhi kadi ya CCM  Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustine Ndugu Simon Philbert Macheyeki ambaye amejiunga rasmi na CCM,katika mkutano huo zaidi ya wanafunzi 86 wa chuo hiko wamejiunga na CCM na wanachama wapya 420 wamejiunga na CCM.
 Kadi za wanachama wapya waliojiunga na CCM kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustine Mwanza.
 Wanachama wapya 420 wajiunga na CCM kutoka Chuo Kikuu cha SAUT Wilaya ya Nyamagana.
 Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo cha Mtakatifu Agustine Ndugu Simon Philbert Macheyeki akila kiapo cha kujiunga na CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Nyamalango wilayani Nyamagana.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na wananchi na wanachama wa Tawi la CCM SAUT Kambarage Mwanza.
Wanachama wa Tawi la CCM SAUT wakiburudisha kwa kucheza na kuimba nyimbo mbali mbali.
 Nifuraha kwa kila Mwana CCM SAUT wakati wa mapokezi ya Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Ndugu Nape Nnauye.
Ujumbe kutoka kwa Tawi la CCM SAUT

No comments:

Post a Comment