Wednesday, May 7, 2014

SHABIKI ALIYE MTUPIA NDIZI DANI ALVEZ APEWA ADHABU KALI

 
alves28apr14-472815 
Ligi kuu ya Hispania (LFP) imeipa adhabu klabu ya Villareal kutokana na kosa la shabiki wao kumfanyia vitendo vya kibaguzi mchezaji wa FC Barcelona mbrazil Dani Alves.
LFP imeiadhibu Villareal kwa faini ya 12,000 euros ($16,000) baada ya mmoja wa mashabiki wao kumtupia ndizi beki huyo wa Barcelona kwenye mchezo baina ya timu hizo uliopigwa kwenye dimba la El Madrigal.
Tukio hilo lilotokea kwenye mchezo ulioisha kwa sare ya 1-1 lilitengeneza vichwa vya habari ulimwenguni kote, kupelekea watu wengi kupiga picha wakiwa wanakula ndizi kuonyesha kupingana na matukio ya ubaguzi wa rangi.
Shabiki huyo wa Villarreal ambaye tayari kafungiwa maisha na klabu hiyo kwenda uwanjani kuangalia mpira.

No comments:

Post a Comment