Friday, May 2, 2014

RAIS KIKWETE AMKABIDHI ZAWADI MFANYAKAZI BORA WA MWAKA KUTOKA MFUKO WA PENSHENI WA PPF, HERMAN KACHIMA KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI‏


Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio (Kushoto), akimsikiliza kwa makini, Naibu Katibu mMkuu wa Wizara ya Habari, Vijana na Michezo, Profesa Ole Gabriel, wakati wa maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo.


Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 5, Herman Kachima, ambaye ni Msimamizi wa huduma kwa wateja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo.
 


Baadhi ya wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF wakiwa kwenye maandamo ya kuingia katika Uwanja wa Uhuru Hapo jana katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.
 


 
Wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF wakipita mbele ya jukwaa kuu.


Meneja Masoko na Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Lulu Mengere (Kulia) akijadiliana jambo na mmoja wa wafanyakazi bora wa mwaka katika sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika Jana Katika Uwanja Wa Uhuru, Jijini Dar Es Salaam. Nyuma ni Mfanyakazi Bora wa Mwaka Kutoka Mfuko wa Pensheni wa PPF, Herman Kachima (wa kwanza Kulia).

No comments:

Post a Comment