Friday, February 28, 2014

SOMA WALICHOSEMA BAADHI YA WASANII KUHUSIANA NA ISSUE YA PNC NA OSTAZ JUMA


Cjapendezwa ata kidogo Na kitendo alichofanyiwa msanii uyu PNC Na Ostadh Juma Na musoma baada ya kwenda kumuomba samahan! Ichi ndicho alichofanyiwa kupigishwa magoti Na kupigwa Picha Na kurecodiwa clip ya video. Tazama Picha hii we kama shabiki Wa bongo fleva huu c udharirishaji? Huu c utumwa kabisa? Mziki ulikuwa ni sehem ya vijana wenye vipaj kujipatia ajira nw unaelekea kuwa sehem ya wapenda CFA wachache wenye visent vya magumash kuwanyanyasia vijana wadogo waliotoka kwnye familia za kimaskini Na Vipaj vyao! Je we kama shabiki Wa msanii uyu maarufu kwa hali hii unayoiona hapo utamueshm kweli Na kumpa thaman kama zaman? Au we kama Ndo ungekuwa msanii uyo baada ya kufanywa hvyo, uyo jamaa anaweza kuwa boss wako kweli? Cwez kumlaumu PNC kwa sbb ana kitu Ndo maana alikubali kufanywa hvyo! Ila we ungependa kuona mziki Wa bongo fleva Na wasanii wanaojipatia majina makubwa nchini mwishon wakiishia kufanywa HV Na wapenda CFA? @sammisago @bongo5 @hassbaby @dogojanja @djchoka @DarTalk @kingkapita

adamjumanxl Sanaa ina thamani gani katika jamii? Wengi wanaichukulia sanaa kama upotezaji muda tu, wengi hawaithamini sanaa kabisa. Na sizungumziii sanaa ya kuimba tu bali sanaa zote, hata kupiga filamu, kutaarisha mziki au uchoraji ni moja ya sanaa na inahitaji umahiri. Jamii yetu kwa ujumla haitupi sifa wanasanaa tunazostahili, sipendi mtu akinichukulia mimi kama “ MPIGA VIDEOOO” huku akiongea na mimi kwa fedheha kisa anauwezo wakulipa, kamwe huwezi kumlipa msanii naomba litambulike hilo. Pia litambulike kuna watu wameeacha kazi zao ambazo walipata mpaka madegree wakaamua kufanya sanaa, kwahiyo sio kila anayefanya sanaa ana njaa au anafanya kwa shinda. Mimi binafsi maisha yangu na yafamilia yangu yaendeshwa kwa kutumia sanaa. Mtu akinidharau kamwe sifanyi nae kazi hata kama anamipesa Hivi leo polisi akitukanwe hadharani kutakua na usalama, polisi wengine hawatakubali? Hivi mtu amdhalilishe dereva wa boda boda unafikiri ni sawa? Kwanini mtu amdhalilishe msanii alafu wana sanaa wote mnakaa kimya kama hayawahusu vile. Mimi PNC sio msanii wangu, lakini naheshimu kazi zake na jitihada zake kama msanii, mimi kama msanii naamini yeye kama msanii amepitia changamoto mpaka amefikia hapo alipo. Naamini huyu msanii ana wazazi, ndugu, jamaa na marafiki wanamtazama, hivi wanamchukuliaje huyu msanii kwa kudhalilishwa mbele ya umma. Baada ya kupata taswira hiyo vuta picha nyingine wanaichukuliaje sanaa kwa ujumla kama mtu anaweza akamfanya msanii hiyvo na asifanywe lolote, maana yake ni sanaa haina thamani. OSTADHI JUMA umeikosea sanaa, umewakosea wanasanaa wote na kama wewe ni msanii basi hustahili sifa hiyo ya usanii. Muombe radhi huyo kijana na jamii nzima ili ulinde heshima yako iliyobaki na heshima ya sanaa kwa ujumla.
SHUKA CHINI KUTOA MAONI YAKO TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment