Monday, February 24, 2014

SABABU ZA LADY JAY DEE KUJIFUNZA KARATE HIZI HAPA.

Moja kati ya surprises zilizokuwepo wiki iliyopita ni pamoja na habari ya Lady Jay Dee aka Anaconda kujifua kikomando kuumudu mchezo wa Karate, habari iliyoambatana na picha zikimuonesha akifundishwa mchezo huo tena akiwa ndani ya mavazi rasmi.

Itakuwaje Jide akishakuwa fiti kwenye mitindo hatari ya karate kama Shotokan, Wado-ryu, Shito-ry na Goju-ryu? Na je, anataka kumkabili nani hasa? Haya ni kati ya maswali ambayo wengi tulijiuliza.
“Kwa sababu ninao muda wa ziada, halafu kukaa tu idol bila kufanya kitu saa zingine inaweza kupelekea mawazo yako kufikiria vitu vibaya. Kwa hiyo nikaona sio vibaya nikifanya mazoezi.” Alisema Lady Jay Dee aka Anaconda.

Alipoulizwa kama kuna mtu anataka kupigana naye alisema hakuna mtu ila anajiweka fiti tayari kwa lolote
“Hapana ni kutaka kujiweka fiti unajua kufanya mazoezi sio kwa ajili ya kutaka kupigana na mtu, ni wewe mwenyewe tu uwe vizuri ili jambo likitokea ujue jinsi ya kuji-protect.” Ameeleza. Mkali huyo wa Joto Hasira amedai kuwa ana mwalimu mzuri na kwamba yeye pia ni mwanafunzi mwenye bidii


Msanii wa muziki kutoka nchini Tanzania, Judith Wambura ei kei ei Lady JayDee amepost baadhi ya picha kupitia ukurasa wake wa Facebook zinazomuonyesha akifanya mazoezi ya mchezo wa ngumi aina ya Karate kwenye kituo kimoja kinachotoa mafunzo hayo hapa jijini Dar es salaam, ingawa bado hajaweza kufahamika wazi kama msanii huyo ameanza rasmi kujifunza mchezo huo ambao ni maarufu na unaopendwa na watu wengi sana Duniani, unaweza ukatazama picha hapo chini.


















No comments:

Post a Comment